KAMATI ya Bunge kuhusu Utangazaji na Maktaba sasa inapendekeza kuwa
wabunge wote 349 wanunuliwe vipakatalishi za matumizi katika mikutano yao kupitia
mitandaoni.
Kamati
hiyo inapendekeza kwamba wabunge wanunuliwa aina ya kisasa ya laputopu kwa jina
Apple MacBook Pro, ambayo inaweza kugharimu hadi Sh105,000 kila moja.
Hii
ina maana kuwa ikiwa mapendekezo hayo yataidhinishwa na wabunge, ununuzi wa mitambo
hiyo utamgharimu mlipa ushuru Sh105 milioni ikizingatiwa kamati hiyo
inapendekeza Spika wa Bunge la Kitaifa Justin Muturi pia anunuliwe
kipakatalishi cha aina hiyo.
Photo:Courtesy
Huenda
mlipa ushuru akagharimika zaidi ikiwa maseneta 68 pia watapendekeza wanunuliwe
vipakatalishi kwa gharama ya mlipa ushuru.Ripoti hiyo ya kamati ya Utangazaji iliyowasilishwa bungeni wiki jana, ilisema kuwa wabunge wanapendelea kutumia vipakatalishi katika mikutano yao ya mtandaoni badala ya iPad.

No comments:
Post a Comment